RAIS MAGUFULI KUFANYA ZIARA YA SIKU 5 MKOANI IRINGA

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Amina Juma Masenza akizungumza na Waandishi wa habari Ofisini kwake

Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa

Afisa habari Mkoa wa Iringa Denis Gondwe(Kulia) pamoja na waandishi wa Habari wa Mkoa huo

Na Dajari Mgidange, Iringa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi Mkoani Iringa kuanzia kesho tar 29 mwezi huu mpaka tar 4 mwezi wa tano mwaka huu.

Katika taarifa yake na waandishi wa habari na Mtandao huu dmgidange.blogspot.com Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Amina Juma Masenza amesema kuwa wanatarajia kumpokea Rais Magufuli jumapili ya tarehe 29 mwezi huu kuanziaa saa 3 asubuhi katika kijiji cha Ndolela Wilaya ya Iringa ambapo atasomewa Taarifa ya Mkoa sambamba na kuzindua Barabara ya kutoka Kijiji cha Migori kwenda Fufu ambayo pia inakatiza mjini Iringa.

“Tarehe 1 mwezi Mei Rais Dr John Pombe Magufuli atakuwa Mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Mei Mosi ambapo Kitaifa yanafanyika Mkoani hapa na kutakuwepo na viongozi mbalimbali akiwemo waheshimiwa Spika wa Bunge na Naibu wake, Mheshimiwa Waziri Mkuu, Waheshimiwa wabunge na wengine wengi”. Amesema Masenza.

Wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Mei Mosi mkuu huyo wa Mkoa wa Iringa amewaomba wananchi wote kujitokeza kwa wingi na kuwahi mapema asubuhi kumlaki Rais Magufuli katika uwanja wa samora mjini Iringa ambapo maadhimisho hayo yatafanyika uwanjani hapo.

Aidha katika Ziara nyingine Tarehe 2 mwezi wa tano mwaka huu Rais Magufuli ataweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Hospitali iliyopo wilayani Kilolo ambapo Pia Masenza amewataka wananchi wa Kilolo kujitokeza kwa wingi katika uwekaji wa jiwe la msingi katika Hospitali hiyo ya Wilaya.

Kadhalika tarehe 3 mwezi huu siku inayofuata Rais Magufuli atazindua kiwanda cha Silverlands ikifuatiwa na uzinduzi wa barabara ya Iyovi Mafinga katika eneo la Ihemi Wilaya ya Iringa vijijini.

Baada ya Ziara hizo Rais Magufuli anatarajiwa kuondoka Mkoani Iringa tarehe 4 mwezi wa tano mwaka huu.

Ujio wa Rais Magufuli Mkoani Iringa ni wa kwanza tangu achaguliwe na wananchi kuwa Rais mwaka 2015.


TAARIFA ZINGINE ZINAZOENDELEA KUSOMWA 


Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment