AFARIKI DUNIA AKIJIPIGA SELFIE MTONI NA KUTUMBUKIA


Kijana mmoja ambaye hakujulikana jina mara moja nchini Nigeria amefariki dunia baada ya kutumbukia mtoni wakati akijaribu kujipiga picha kwa simu maarufu kama 'Selfie'.

Tukio hili limetokea eneo la Nembe katika mji wa Bayelsa, ambapo kijana huyo alikua anajaribu kupiga picha ya mwisho ya kumbukumbu katika chuo cha mafunzo ya usalama NYSC.

Wakisimulia tukio hilo baadhi ya mashuhuda wamesema kwamba mtu huyo aliteleza kwa bahati mbaya wakati walipokuwa amesimama eneo la “Jetty” katika mto huo na kutumbukia mtoni.

Mwili wa kijana huyo ulipatikana dakika 30 baada ya kuzama na hakuna taarifa za kumtambulisha mtu huyo.


Mamlaka za mji huo zimeshindwa kumtambua mtu huyo na hakuna ndugu wala jamaa ambaye amekwisha jitokeza hata baada ya picha za mtu huyo kusambaa katika mitandao ya kijamii.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment