NONDO ATAKA ABADILISHIWE HAKIMU


 Mwanafunzi Abdul Nondo ameiandikia barua Mahakama ya Iringa kuomba kubadilishiwa mwendesha mashtaka wa kesi yake Hakimu John Mpitanjia.

Nondo ambaye anashtakiwa kwa makosa mawili ya kudanganya kutekwa na kutoa maelezo ya uongo kituo cha Polisi Mafinga, amesema kuwa haridhishwi na mwenendo wa kesi yake na anazo hoja 5 ambazo ameziwasilisha mahakamani hii leo kuomba kubadilishwa kwa hakimu.

Amesema amekuwa akimuona Hakimu Mpitanjia akiwa na RCO wa wakiwa ofisini na kupanda gari lake jambo ambalo limepelekea yeye kuhisi kwenda tofauti na kesi yake Mahakamani hapo.

Sababu nyingine amesema kuwa Hakimu huyo amekuwa akimuuliza shahidi namba tatu upande wa Jamhuri kuhusu mawasiliano yake na shahidi huyo hali ambayo anatilia shaka kutotendeka kwa haki katika kesi hiyo.
Upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na Wakili wa Serikali Abel Mwandalamo ameiomba Mahakama kutupilia mbali maombi hayo kutokana na kukosa ushahidi wa maombi yaliyoelezwa na upande wa utetezi.

Hakimu Mpitanjia amesema kuwa amesikiliza pande zote mbili na amehairisha kesi hiyo mpaka Tarehe 16 ya mwezi huu ambapo atakuja na majibu ya kutoendelea kusikiliza kesi hiyo au la.

Naye Mratibu wa haki za Binadamu Nchini Onesmo Olengurumwa amesema mtuhumiwa Abdul Nondo anayo haki kisheria kuomba kubadilishiwa mwendesha mashtaka endapo anahisi kutotendeka kwa haki wakati wa kesi yake.
 


Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment