ALIYEKUWA MPENZI WA NONDO ATOA USHAHIDI MAHAKAMANI



Kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) Abdul Nondo imehairishwa leo mpaka tar 27 mwezi huu kutokana na upande wa Jamhuri kuomba muda wa kujibu hoja za upande wa Utetezi.

Hatua hiyo imekuja mara baada ya upande wa Jamhuri kuiomba Mahakama kupokea kielelezo cha ushahidi wa nakala ya mawasiliano yaliyokuwa kwenye simu ya Nondo.

Upande wa Utetezi ukiwakilishwa na Wakili Jebrah Kambole ulipinga kupokelewa kwa kielelezo hicho  kutokana na kielelezo hicho kuambatanishwa na taarifa za kwenye simu pamoja na Laptop huku ilipaswa kuambatanishwa taarifa za kwenye simu pekee yake.

Sababu nyingine ambayo upande wa Utetezi imepinga ni kutokana na vielelezo hivyo kutokidhi vigezo vya Kisheria ya Electronic Transaction act ya 2015 Kifungu kidogo cha 18
Aidha kwa upande wa Jamhuri umeombwa kuhairishwa kwa shauri hilo ili kuweza kujiridhisha na hoja zilizotolewa na upande wa utetezi.

Naye mwendesha mashtaka wa kesi hiyo Hakimu John Mpitanjia  alikubali ombi hilo na kuhairisha kesi hiyo mpaka tare 27 mwezi huu.

Awali Mahakama ilisikiliza ushahidi kutoka upande wa Jamhuri Veronica Sylivester Fredy aliyekuwa mpenzi wa Nondo ambaye alikili kumtambua Nondo kuwahi kuwa Mpenzi wake lakini waliachana mwaka jana 2017.

Shahidi wa pili ni Detective Abdulkarim ambaye yupo Makao makuu ya Polisi Dar Es Salaam kitengo cha uchunguzi wa makosa ya kimtandao ambaye ndiye aliyetoa kielelezo cha nakala ya taarifa zilizokuwemo kwenye simu ya Nondo.


Itakumbukwa kuwa Nondo anatuhumiwa kwa makosa mawili Kosa la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni Machi 7, 2018 akiwa Ubungo na kusambaza kwa kutumia mtandao wa WhatsApp kuwa yupo hatarini.

Kosa la pili ni kutoa taarifa za uongo akiwa mjini Mafinga kwa askari Polisi wa kituo cha Mafinga Wilayani Mufindi.


Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment