KLOPP AWATAKA MASHABIKI WA LIVERPOOL KUWAHESHIMU ROMA



Na Dajari Mgidange,



Kocha wa timu ya majogoo wa jiji Liverpool amewataka mashabiki wa timu hiyo kutumia busara kubwa wakati wa mapokezi ya timu wanayokutana nao kwa mara ya kwanza mchezo wa nusu fainali ya mabingwa barani ulaya Roma.

Hatua hiyo imekuja mara baada ya michezo iliyopita dhidi ya Manchester City katika hatua ya Robo fainali walipokutana mahasimu hao wakati wa mapokezi ya timu hiyo Anfields mashabiki wa Liverpool walirusha chupa za vinywaji na baruti za moshi.

Klopp amewataka mashabiki kuwaonesha heshima Roma na kuleta vurugu zozote zile hata kurusha vitu viatavyowavunjia heshima.

“Hatuhitaji kurusha vitu vyovyote vile hii Club inaonekana ni kutoka anga la maajabu zaidi tutafanya vizuri ndani ya uwanja na nje ya uwanja tunahitji kuonesha heshima tunayotakiwa kuonesha”. Amesema Klopp

Katika tukio lililofanyika tarehe 4 Mwezi huu dhidi ya Manchester City baadhi ya Polisi pia walijeruhiwa kutokana na vurugu za mashabiki Liverpool lakini bado tukio hilo linaendelea kufanyiwa uchunguzi.

Liverpool ni timu pekee ya Uingereza iliyobakia katika michuano mikubwa zaidi Duniani ya Uefa Champions na watahitaji ushindi leo wakiwa nyumbani Anfield dhidi wa wageni wao Roma mchezo utakaopigwa majira ya saa 3:45 usiku.

Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment