KESI YA NONDO YAHAIRISHWA KUTOKANA NA MVUTANO WA MAWAKILI

Nondo katikati akiwa na mawakili wake



Na Dajari Mgidange,

Mashahidi wawili kati ya watano waanza kusikilizwa katika kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) Abdul Nondo huku kesi ikihairishwa kutokana na mvutano wa mawakili.

Kesi hiyo ambayo leo mahakama imeanza kusikiliza upande wa mashtaka ambao wamewaleta mashahidi watano sambamba na vielelezo vya ushahidi na upande wa utetezi ulikuwa tayari kusikiliza.

Mashahidi wawili kati ya watano walioletwa na upande wa mashtaka uliowakilishwa na Wakili wa Serikali Alex Mwita akisaidiwa na Wakili Pienzia Michombe walipata nafasi ya kuanza kusikilizwa ushahidi wao.

Mashahidi hao wawili waliopata nafasi ya kutoa ushahidi ni wote kutoka Kituo cha Polisi cha Mafinga Wilayani Mufindi ambao ni E.2328 Copro Salum ambaye alimpokea Nondo na kuandika maelezo yake na Mwingine ni E.7651 Copro John ambaye ni Afisa upelelezi wa Kituo hicho.

Shahidi wa kwanza ambaye ni Copro Salum katika kutoa ushahidi wake amesema kuwa Mnao Tar 7 machi mwaka huu majira ya saa nane mchana aliingia kazini chumba cha mashtaka na akiwa hapo akiendelea na kazi ndipo majira ya saa moja usiku alikuja mteja aliyejitambulisha kuwa anaitwa Abdul Mahmudu Nondo akiwa katika hali ya kawaida akiwa na Begi na mfuko wa Rambo na kumueleza kuwa alitekwa na watu wasiofahamika.

Aidha baada ya hapo Copro Salum amesema kuwa alichukua jukumu hilo na kukabidhi kwa afisa upelelezi kituoni hapo Detective John kwaajili ya kumhoji kwa kina.

Kwa upande wake Shahidi namba mbili Copro John  amesema kuwa Mnamo tar 7 mwezi Machi majira ya saa Moja jioni alipokea maelezo kutoka kwa copro Salum kuwa kuna kijana ameleta malalamiko kuwa ametekwa ndipo alipochukua jukumu la kumhoji kwa undani zaidi.

Amesema baada ya kuona swala hilo ni gumu alichukua jukumu la kumpeleka ofisi ya mkuu wa Upelelezi ambako aliamriwa kupekua mabegi ya Nondo na kukuta kompyuta ndogo ya Laptop aina ya Dell, Simu aina ya Itel, Kadi ya Benk na Kitambulisho cha Chuo.

Kesi hiyo imehairishwa mpaka Jumatatu ya Tarehe 23 Mwezi huu kutokana na Upande wa Utetezi chini ya Wakili Jebra Kambole na Wakili wa Serikali Alex Mwita kuwa na mvutano juu ya utofauti wa majina yaliyoandikishwa na Copro John na Copro Salum kuambatanishwa kama vielelezo vya ushahidi mahakamani.

Itakumbukwa kuwa Nondo anatuhumiwa kwa makosa mawili Kosa la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni Machi 7, 2018 akiwa Ubungo na kusambaza kwa kutumia mtandao wa WhatsApp kuwa yupo hatarini.

Kosa la pili ni kutoa taarifa za uongo akiwa mjini Mafinga kwa askari Polisi wa kituo cha Mafinga Wilayani Mufindi.







Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment