KESI YA NONDO YAPIGWA KALENDA

Abdul Nondo akiwa Mahakamani leo April 18

Mawakili wa Nondo Jebra Kambole Kulia na Chance Mloga katikati



Kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) na Mwanafunzi wa UDSM Abdul Nondo ambayo ilipaswa kusikilizwa mfululuizo leo April 18, 2018 na April 19 imehairishwa mpaka kesho kutokana na Hakimu wa kesi hiyo kuwa na kesi nyingi.

Mmoja wa mawakili wa Nondo wakili Chance Mloga amesema kuwa Hakimu John Mpitanjia aliomba kupumzika kutokana na uwingi wa kesi alizozisikiliza siku ya leo.

Amesema wamekubaliana Kesi hiyo kusikilizwa tena kesho April 19, 2018 mapema asubuhi huku upande wa Jamhuri tayari ukiwa umeleta mashahidi wanne wa kesi hiyo.

Nondo anatuhumiwa kwa makosa mawili Kosa la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni Machi 7, 2018 akiwa Ubungo na kusambaza kwa kutumia mtandao wa WhatsApp kuwa yupo hatarini.

Kosa la pili ni kutoa taarifa za uongo akiwa mjini Mafinga kwa askari Polisi wa kituo cha Mafinga Wilayani Mufindi.


Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment