LIPULI FC 1-1 SIMBA SC, ADAM SALAMBA AENDELEZA UBABE

Mchezaji wa Lipuli Fc Adam Salamba akipokea hundi ya sh. millioni moja

Salamba akipokea king'amuzi cha Azam

Bench la Ufundi la Simba wakishuhudia Mpambano

Mashabiki wa Simba wakishangilia mpambano


Simba wakishambulia lango la Lipuli

Mashabiki wa Lipuli Fc wakishangilia bao lililofungwa na Adam Salamba


Timu ya Lipuli Fc imelazimishwa sare nyumbani na Simba Sc ya 1-1 katika Dimba la uwanja wa Samora mjini Iringa.

Simba walionekana kupooza kipindi cha kwanza ambapo walilazimishwa na mashambulizi ya Timu ya Lipuli kufika golini kwao.

Mchezaji bora wa Lipuli wa Mwezi machi Adam Salamba akadhihirisha ubora wake kwa kuweza kupachika bao dk ya 31 ya mchezo katika kipindi cha Kwanza cha mchezo na kufanya lipuli kuongoza kipindi cha kwanza hadi kinamalizika.

Kipindi cha Pili Simba walirudi katika hali tofauti na kuanza kushambulia kwa nguvu na kulazimisha mashuti kufika katika lango la Lipuli na hadi kufikia dk ya 66 Laudit Mavugo akaisawazishia Simba.

Dakika 90 zikamalizika na timu hizo zote mbili zikitoka sare ya kufungana bao 1-1  
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment