DANTE APEWA UKAPTENI KWA MARA YA KWANZA YANGA



Beki wa klabu ya Yanga, Andrew Vincent 'Dante' jana alipewa mikoba ya kuwa kapteni wa timu hiyo kufuatia kutokuwepo kwa Kelvin Yondani pamoja na Nahodha Mkuu, Nadir Haroub 'Cannavaro'.



Dante amefanikiwa kupata fursa ya kupata majukumu hayo ya Ukapteni wa muda, ikiwa ni katika mchezo kimataifa wa kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya U.S.M Alger ambao ni wa kwanza kwake.

Nafasi hiyo hutumiwa mara nyingi na Kelvin Yondani kama msaidizi inapotokea Nahodha mkuu, Cannavaro hajaanza.

Baada ya mchezo huo kumalizika jana, Yanga inatarajiwa kuwasili nchini kesho ambapo imeanza safari ya kurejea Dar es Salaam leo.

Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment