UKOSEFU WA OFISI YA MGAMBO MWENYEKITI ALALA NA WATUHUMIWA NYUMBANI KWAKE

Picture

MTENDAJI   wa  kijiji  cha  katili    kata  ya  samazi   wilaya   ya
Kalambo mkoani  Rukwa Oska  Sauloni  amejikuta  kwenye  wakati  kwenye
  wakati mgumu  na kugeuza  nyumba    yake  kuwa   mahabusu  ya
kuhifadhia  watuhumiwa  sambamba  na  kufanyia  kazi   za  ofisi
nyumbani  kwake  kutokana na  kijiji  hicho  kuwa  na  ukosefu  wa
ofisi   tangia   nchi    Tanzania  kupata   uhuru mwaka  1961


 Kijiji cha   katili  kina  jumla   ya    kaya   282 na  wananchi  500
ambapo  kati  yao   nguvu   kazi  ni  wananchi  370   ambapo  wananchi
wake  wanajihusisha  na   shughuri  za  kilimo  na  uvuvi   kupitia
ziwa   Tanganyika.

 Hata   hivyo    kijiji  hicho  kina  ukosefu   wa   ofisi  ya  kijiji
, ambapo  waharifu   wanalazimika  kufungiwa  kwenye  nyumba  ya
mtendaji  wa  kijiji  hicho  na  huku  wengine   wakilazimika  kulala
na  mtendaji   kitanda kimoja     kutokana na  kijiji  hicho  kuwa
na  ukosefu  wa   ofisi  na mahabusu  ndogo   ya  kuhifadhia
watuhumiwa ambao  wamekuwa  wakikamatwa   na  huku    makao  makuu
ya  kituo   cha  polisi  wilayani  humo  yakiwa    zaidi  ya  umbali
wa  km  30 kutoka  kijiji  husika.

Mtendaji   wa  kijiji hicho Osika  sauloni ,amesema  analazimika
kugeuka  kuwa  mgambo   wa  kijiji    kwa  kulala  na  watuhumiwa
kitanda kimoja  nyumbani  kwake  ikiwemo  kulazimika   kufanyia  kazi
za  ofis  nyumabani  kwake  kutokana na  kijiji  hicho  kuwa  na
ukofu   wa   ofis hali  ambayo  imekuwa  ikimpa  wakati  mgumu
hususani  nyakati  za  usiku  pindi  wtuhumiwa   wanapo  kuwa
wakileta   fujo  na  kutaka  kumpiga.

 Mwenyekiti  wa kijiji  hicho ,Helmani  Chitu ,ambae  licha  ya
kukili  kuwep[o  adha  hiyo,  licha  hilo  kijiji  chake  kina
kabiliwa  na  chanagamoto  nyingi  ikiwemo  ukosefu  wa  shule  ya
msingi  na  zahanati  na  kusema   kwa  sasa  wameanza  ujenzi  wa
shule  ya  msingi   hivyo  wakimaliza   hilo  ndipo  wataanza  kujenga
 ofis  na mahabusu.

Mtendaji   wa  kata  hiyo  Tedsoni  Chonya  amesema  wananchi wameanza
 kufyatua  tofari  kwa  lengo  la  kukabiliana na  chanagamoto  hiyo.

Diwani  wa  kata  hiyo   Juma  kibongwe amesema  ametoa  maagizo  kwa
mwenyekiti   wa  kijiji  hicho   dhidi  ya  kuhamasisha  wananchi
kujenga  ofis   ya  mtendaji  ili  kuondokana  na  adha  anazo
kabiliana  nazo.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment