ACHOMEWA NYUMBA KUTOKANA NA WIVU WA KIMAPENZI


 

Mnamo tarehe 05/03/2017 majira ya saa o5:30 usiku huko maeneo ya
Mafulala, kata ya Majengo, tarafa ya Lwiche, Manispaa ya Sumbawanga na
Mkoa wa Rukwa.

MKAZI mmoja  wa  Kata  ya  majengo  mweye  umri  wa  miaka  26, Malia
kokolo ,amejikuta  kwenye  wakati  mgumu  baada   ya  kuchomewa
nyumba  yake  na  Joel  Mwenga , Mwenye umri wa miaka 48, Mndali,
Mkazi wa Mafulala. Kutokana  na  wivu  wa  kimapenzi.

Kamanda   wa  polisi mkoani  Rukwa Geoge  Simba  kyando amesema
Chanzo cha kufanya hivyo ni wivu wa mapenzi ambapo mlalamikaji alienda
kuulizia sababu za EMMANUEL MWENGA ambaye ni mtoto wa mtuhumiwa
kutangaza kuwa na uhusiano wa kimapenzi  na mlalamikaji.

Mbinu iliyotumika ni kwamba mtuhumiwa amekamatwa alimvizia mlalamikaji
akiwa amekimbia baada ya ugomvi kutokea ndipo akachoma nyumba.

Mtuhumiwa amekamatwa na atafikishwa mahakamani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa Kamishna Msaidizi wa Polisi GEORGE
SIMBA KYANDO   anatoa rai kwa wananchi kuacha kujichukulia sheria
mkononi  na kuwashauri kupeleka migogoro yao sehemu husika ili waweze
kusaidiwa kuitatua kuliko kuchukua maamuzi magumu kama hayo.
Aidha anatoa onyo kwa wananchi kuwa makini kwani hatawafumbia macho
wale wote wanaofanya uhalifu.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment