LEO NI SIKUKUU YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR

LEO ni siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, zilizoungana miaka 54 iliyopita. Maadhimisho hayo yanaendelea kwenye uwanja wa Jamuhuri mjini Dodoma. Sherehe hizo zinapambwa na mgeni rasmi, Amri Jeshi Mkuu wa Majeshi la Ulinzi na Usalama, Rais John Magufuli na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein. Siku hii ni kumbukumbu ya kuzaliwa Tanzania baada ya nchi hizo mbili kuungana pamoja na wananchi wa pande zote mbili.
Maadhimisho ya mwaka huu ni ya 54 tangu kuzaliwa kwa Tanzania na ni mara ya pili mfululizo, kufanyika katika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.
Katika maadhimisho hayo ya mwaka jana, mgeni rasmi alikuwa ni Rais Magufuli.
Aprili 26, 1964 waasisi wa taifa hili, Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Abeid Amani Karume waliunganisha nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar, kwa kuchanganya udongo wa pande hizo mbili.
Kwa miaka mingi maadhimisho hay,a yalikuwa yanafanyika katika Uwanja wa Uhuru (Shamba la Bibi) jijini Dar es Salaam.
Lakini tangu Rais Magufuli aingie madarakani, huu ni mwaka wa pili mfululizo yanafanyika Dodoma, mahali ambapo ni makao makuu ya nchi.
Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu inasema Muungano huu ni wa mfano pekee duniani: Tuulinde, Tuutunze, Tuuimarishe na Kuudumisha kwa maendeleo ya Taifa letu".

Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment