Jaji wa mahakama kuu India ahukumiwa

India Jaji CS Karnan 
Aliyekuwa hakimu wa zamani wa mahakama kuu nchini India amepelekwa lupango Mashariki mwa mji wa Kolkata, siku moja baada ya kukamatwa kwake Kusini mwa mji wa Tamil Nadu.

Jaji C.S. Karnan alikuwa akijitahidi kujificha kuepuka mkono wa kisheria dhidi yake tangu mahakama kuu ilimhukumu kifungo cha miezi sita jela mnamo mwezi uliopita kwa kosa la dharau dhidi ya mahakama.

Jaji Karnan kwa sasa amevuliwa mamlaka yake ya mahakama. Na inaelezwa kuwa ndiye jaji wa kwanza nchini humo kutoka mahakama kuu kuhukumiwa na kufungwa jela.

Jaji huyo alihojiwa baada ya kumwandikia waraka waziri mkuu,baada ya matamshi yake dhidi ya majaji wenziwe wa mahakama kuu kuwa ni wala rushwa waliopitukia.
 
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment