ZAIDI YA WAGONJWA 33 WAMEPATIKANA NA TEZI DUME MKOANI IRINGA




Tezi dume ni ugonjwa unaopatikana katika njia ya mkojo ndani ya mwili wa binadamu na mara nyingi huwapata wanaume wa miaka kuanzia 40 na kuendelea.

Ugonjwa huu umekua ukishika kasi kwa hivi karibuni kutokana na wanaume wengi kupatikana wakiwa na huu ugonjwa ambao umekua gumzo kwa miaka ya hivi karibuni ambapo wanaume wengi wenye umri wa mtu mzima kuanzia miaka 40 na kundelea wameripotiwa kuwa na tatizo hili.

Watu wengi hawana uelewa wa ugonjwa huu na huku wengine wamekua wakisema tezi dume ni sawa ugonjwa aina ya Busha huku wengine pia wakiwa na imani potofu kua ugonjwa huu hupatikana kwa kurogwa.

Daktari Mseleto Nyakiroto ni Daktari bingwa wa magonjwa ya upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoani Iringa ambaye MATUKIO DAIMA ilifika ofisini kwake kuweza kufahamu juu ya ugonjwa huu wa tezi dume ambao umekua gumzo miaka ya karibuni na ulianza kufahamika zaidi baada ya Mh Rais Mstaafu DR  Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2014 kuupata ugtonjwa huo na kwenda kutibiwa huko nje ya nchi nchini Marekani.

“Tezi dume si ugonjwa ila Tezi dume linapopata tatizo ndio hutokea huo ugonjwa na huwapata zaidi wanaume ambao hupatikana katikati ya kibofu na njia ya mkojo ndani ya mwili wa mwanume na linapovimba mgonjwa hupata shida ya kuweza kukojoa na wakati mwingine huziba kabisa na mkojo kushindwa kupita”. Alisema Dr Nyakiroto.
 
Daktari amebainisha sababu mbalimbali ambazo zinasababisha kuupata ugonjwa huu ambayo ni homoni za mwanaume zikiwa kwa wingi sana husababisha ugonjwa wa Tezi Dume huku pia kurithi kutoka baba mzazi huweza kusababisha mtu kuweza kupata ugonjwa huu na dalili zake Nyakiroto anaeleza ni kua na matatizo yakushindwa kukojoa vizuri na usiku mgonjwa anakua anakojoa mara kwa mara na hasa kwa watu wazima wakuanzia miaka ya 40 huku wengine wakichelewa kwenda hospitali njia za mkojo huziba kabisa na kushindwa kukojoa .

“Matibabu ya ugonjwa wa tezi dume hutegemea kulingana na hali mhusika na kua kama atakua na uvimbe atafanyiwa upasuaji yaani Operation na kwa wale ambao hawana uvimbe hua tunawapa dawa tu na kuwarusu kwenda majumbani kwao kuendelea kutumia dawa”. Alisema Dr Nyakiroto

Nyakiroto anaeleza njia ya kubaini tatizo baada ya mgonjwa kuwafikia ambayo  mara nyingi watu wengi wanashtuka na wengine kugoma kabisa kupimwa kutokana na aina yenyewe ya upimaji wa gonjwa huu wa Tezi dume kuwa hutumia njia ya haja kubwa kubaini tatizo kwa kuingiza baadhi ya vifaa eneo hilo na kubaini tatizo lakini pia njia nyingine ya kubaini tatizo hilo ni kutumia mashine ya Ultrasound ambayo hupiga picha sehemu yenye tatizo.

Aidha Nyakiroto anaeleza tofauti kati ya ugonjwa wa Tezi dume na Busha na kua tezi dume hutokea ndani ya mwili wa mwanaume katikati ya njia ya mkojo na kibofu na huwapata watu wa umri zaidi ya miaka 40 huku Busha ni ugonjwa unaopatikana maeneo mengi ya Pwani na husababishwa kwa kungw’atwa na mbu ambao hupatikana maeneo hayo ya pwani na ugonjwa huu huonekana kwa macho kwani upo katika korodani za mwanaume punde mwanaume anapopata ugonjwa huu korodani zake huvimba kutokana na kujaa maji.

Idadi ya wagonjwa waliopatikana Mkoani Iringa wenye ugonjwa wa tezi dume tangu mwaka 2016 hadi sasa wamefikia wagonjwa 33 na wote waliweza kutibiwa na wakaweza kupona tatizo hilo.

Sawa na hilo Myakiroto amewaomba wanaume wenye umri zaidi ya miaka 40 ambao wanazo dalili ambazo ameeleza waweze kufika hospiatalini  ili kuweza kuwapata matibabu kwani ugonjwa huo unatibika kabla hawajapata madhara makubwa zaidi.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment