MSAFARA WA WAKALA WA MISITU WAVAMIWA.


Msafara  wa  wakala  wa  misitu   Tanzania    TFS   umevamiwa    katikati  ya  msitu   na  wananchi  wa  kijiji  cha Mau  kata   ya  Mbuluma wilaya   ya  kalambo mkoani  Rukwa kisha  gari  la  msafara   huo  yenye  namba  za  usajili   T. 8212  STK  kupigwa  mawe na  huku mafisa  wa  misitu  wakipotenea  chuchupu   kuambulia  kipigo.

Tukio   hilo  la  kushangaza  limetokea  katika   kijiji  cha  Mau   na   kuvamiwa  na   wananchi   wa  kijjiji  hicho   kwa mawe na marungu   na kuharibu   gari  la  msafara huo .

Akiongea  na  Mtandao huu ofisini  kwake  mara  baada  ya  tukio  kutokea   meneja   wa  misitu TFS  wilayani  humo,  Samweli  Matula  amesema  tukio  hilo  limetokea  wakati  maafisa  misitu wakiwa  wanaelekea  doria , ambapo  wakiwa   kijijini  hapo  walivamiwa  na  kundi  la  wananchi  ambao  walikuwa  wamebeba  mkaa  na  kuvamia  gari   lao  kwa  mawe  na  kupelekea  maafisa  wake  kukimbia   kwa  kuhofia   usalama  wa  maisha  yao.

Amesema  baada  ya  tukio  kutokea  walitoa  taarifa  polisi ambao  walifika  mapema  eneo  la  tukio  na  kukuta  gari   likiwa   limevunjwa  vioo  kwa mawe .
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment