AJIKATA UUME WAKE KUTOKANA NA MISONGO YA MAWAZO,

Jamani mpo tayari kwa picha za tukio la moshi???Mana zinatisha kidogo MKAZI mmoja wa kijiji cha Kate kata ya Kate wilayani Nkasi mkoani Rukwa
Samwel Kambole (64) amenusurika  kifo  baada   ya  kujika kata   uume  wake
baada  ya   kupatwa  na  hasira   nyingi  zilizo  tokana na  misingo   ya
mawazo  inayo  mkabili.

Akisimulia  kutokea   kwa  mkasa  huo    kwa  mashariti  ya  kuto
chukuliwa   sauti  yake mwenyekiti wa kitongoji cha Kotazi kijiji cha Kate
Richard Mselema amesema kuwa mtu huyo aliamua kujikata katika sehemu zake
za siri  akidai kuwa usiku wakati  amelala  alimuota usingizini mke wake
ambaye ni marehemu kwa sasa akifanya naye tendo la ndoa.

Amesema  baada ya kuamka asubuhi hakumuona tena mkewe aliyemuota usiku na
akichanganganya na matatizo mengine yanayomkabili aliamua kuuchukua uamuzi
wa kuanza kuukata uume wake kwa  kutumia   wembe  na baada ya kupata
maumivu makali aliamua kupiga kelele za kuomba msaada.

Amedai  kuwa kele hizo ziliwashitua wakazi wa kitongoji hicho na kwenda
eneo la tukio na kukuta mtu huyo akiwa amejichinja katoka sehemu zake za
siri ambapo walitoa taarifa katika kituo kidogo cha Polisi cha Kate na
kupewa PF3 na kukimbizwa katika zahanati ya Mission ya Kate kwa matibabu.

Mganga wa zamu katika zahanati hiyo Paul Katindi amekiri kumpokea mgonjwa
huyo na kuwa wao kama wauguzi walichukua hatua za haraka kumpatia matibabu
mgonjwa huyo ambapo jitihada zao ni kama ziliweza kuzaa matunda kwa kuweza
kuyaokoa maisha ya mtu huyo.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Nkasi Zeno Mwanakulya  ambae pia  ni
kaka  mtu  na   kijana  huyo, amethibitisha kutokea kwa tukio  na  kusema
chanzo  ni   misongo ya  mawazo  kutokana na  siku  za  hivi  karibuni
kufiwa   na  mkewe   pamoja  na   kupokonywa   mashamaba  yake  yote  na
ndugu  zake  kisha  kuayauza  bila   ushirikishwaji na  kusema  kijana
huyo alitumia  kifaa  aina  ya  wembe kutoa   uume wake.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment