AFARIKI DUNIA KWA KUKATWA NA MASHOKA

MKAZI mmoja  wa  kijiji  cha  loesha  kata  ya  Mbuluma   wilaya   ya  Kalambo mkoani  Rukwa  Regani  Kakusa  miaka  32  ameuwawa  na  watu  wasio  fahamika kwa  kukatwa  na  shoka  sehemu  za  kichwani  kisha  kufariki  dunia  hapo  papo  kutokana na  wivu  wa  kimapenzi.

Diwani  wa  kata  hiyo  saidi manoti  magesa  ,amesema mtu  au  watu  wasio  fahamika   walimvamia    kijana   huyo    kisha  kumkata  na  shoka  sehemu  za  kichwani  na  kupelekea  umauti  wake kumfika.

 Kamanda  wa  pilisi mkoani  Rukwa  Geoge  Simba  Kyando , amesema Chanzo cha kufanya mauaji hayo ni wivu wa mapenzi ambapo inasadikiwa kuwa marehemu alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mke wa  mtuhumiwa na  kusema Mbinu ilotumika kufanya mauaji hayo ni kwamba mtuhumiwa alimvizia kwa nyuma marehemu wakiwa wameongozana kuelekea mnadani.

Aidha  kamnada   kyando  amesema Kamand ametoa  ushauri kwa wananchi hususani wanandoa kuwa waaminifu katika ndoa zao hata pale panapotokea kutokuelewana waende katika taasisi za serikali zinazohusika na masuala ya ndoa ili waweze kutatuliwa matatizo yao kisheria zaidi na sio kuchukua maamuzi magumu ya kuua ambapo ni kosa la jinai kujichukulia sheria mkononi.Aidha ameahidi kumsaka mtuhumiwa popote alipo  ili aweze kushukuliwa hatua  stahiki za kisheria.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment