DAKTARI AKWAMISHA KESI YA SCORPION

 
Ushahidi katika kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kujeruhi inayomkabili, Salum Njwete (34) maarufu Scorpion, umeshindwa kuendelea baada ya upande wa Jamhuri kudai shahidi hakufika.


Sababu za kutofika kwa shahidi huyo ambaye ni daktari kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) ni kutokana na kuwa nje ya kituo chake cha kazi hivyo hakupatikana jana.


Mshitakiwa Scorpion alipandishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, mbele ya Hakimu Mkazi, Flora Haule, wakati shauri hilo lilipopelekwa kwa ajili ya kuendelea na ushahidi upande wa Jamhuri.


Wakili Mwandamizi wa Serikali, Nassoro Katuga, alidai upande wa Jamhuri ulipanga kumhoji shahidi ambaye ni daktari lakini kwa vile alikuwa na dharura ingefaa mahakama impangie tarehe nyingine.


“Mheshimiwa hakimu shauri lilikuja kwa ajili ya kusikilizwa na upande wa Jamhuri ulipanga kumleta shahidi ambaye ni daktari lakini ameshindwa kufika leo, ana dharura ambayo inaweza ikachukua wiki tatu.


“Hivyo kwa mujibu wa kifungu namba 225 cha Sheria ya Mwenendo wa Kesi ya Makosa ya Jinai ambayo inataka kesi isiahirishwe zaidi ya wiki mbili kama mshitakiwa yuko mahabusu, tunaomba mahakama itaje hapa tupange tarehe ya kusikilizwa,’’alisema.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment