WATU WENYE ULEMAVU WA NGOZI ALBINO MKOA WA IRINGA WAPATIWA MSAADA NA ELIMU YA MATUMIZI YA VIFAA

Watu wenye ulemavu wa ngozi yaani ALBINO wamepokea vifaa pamoja na elimu kuhusu matumizi ya vifaa na mafuta ambayo huwakinga na mwanga mkali unaotokana na miale ya jua kali. Hayo yamefanyika leo hii katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa wakati wakipewa maelekezo na jinsi ya kutumia mafuta hayo ya ngozi ambayo yanawalinda kutokana na miale ya jua.
 

 



Katibu wa watu wenye ulemavu (TAS)

Dr Pilly Shing’oma  akitoa maelekezo


Wanafunzi wakipakana mafuta aina ya Kilimanjaro Suncare 

Dr Pilly Shing’oma ni daktari anayehusika na magonjwa ya ngozi na Albino ikiwa ni mojawapo, amesema watu  wenye ulemavu wa ngozi wapo wengi mkoani hapa na mafuta hayo wanayowapa yanauzwa kwa gharama kubwa japo wao wanatoa bure katika clinic zao zote zinazotoa Huduma hizo. Pia Dr. Pilly amewaomba wazazi na walezi pamoja na watu wengine wenye ulemavu huo wa ngozi kujitokeza kwenda katika vituo hivyo vya Afya ili kuweza kupatiwa misaada mbalimbali pamoja na matibabu ya ngozi. Lakini pia Aliongeza kwa kutoa wito kwa wanajamii kuto amini katika imani za kishirikina kwamba viungo vyao vya mwili  kutumika katika kuleta utajiri na kua huo ni uongo ambao unafanywa na baadhi ya waganga wa jadi.
Katibu wa Chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi (TAS) Mkoa wa Iringa bwana Leo Sambala amewashukuru shirika la USAID kuwapatia vifaa vinavyowasaidia kuto athirika na mionzi ya jua wakiwa wanafanya shughuli zao. Aidha katibu huyo amewaomba Walimu kuwasaidia wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi ambao wako mashuleni kutotoa adhabu kali kwa wanafunzi hao kwa kuwaweka juani na pia kuwapa kipaumbele kwa kuwaweka darasani viti vya mbele ili waweze kuona maandishi ambayo yameandikwa na kuwapa notes ambazo zina maandishi ambayo wanaweza kuyasoma kwa urahisi.
Watu wenye ulemavu wa ngozi mkoa wa Iringa wapo karibu 350 ambao wanaishi sehemu mbalimbali za Mkoa huu na baadhi yao wamekua ni vigumu kupatiwa misaada hiyo kutokana na wengine kukaa shemu za mbali na pia hali ngumu ya maisha yao inawafanya kukosa nauli za kuweza kusafiri kuja kuchukua huduma hizo.
Hivi karibuni hakujaripotiwa kuwepo kwa mauaji ya Watu wenye ulemavu wa ngozi yaani ALBINO kuuawa na hii inamaanisha kua elimu imewezqa kuwafikia watu wengi zaidi na wameelimika tofauti na ilipokua mwanzo kulipoku kunaripotiwa  mauaji mengi zaidi ya watu hawa wenye ulemavu wa ngozi.



Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment