JPM ATOA MAAGIZO MANNE BANDARINI

Rais Magufuli  ameagiza mkataba wa kampuni ya Ticts inayopakia na kuondosha mizigo bandarini ufanyiwe marekebisho ili kulinufaisha Taifa kutokana na oparesheni zake bandarini.

Vilevile ameiagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA) inunue mashine nne za kukagulia mizigo inayoingia bandarini hapo.jpm-bandariniAmeitaka TPA na waziri husika kufunga floor meters ndani ya miezi minne.

Pia TPA ijenge bandari kavu Mlandizi na kutozitumia binafsi zilizopo kwakuwa zinatumika kukwepa kodi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa imeeleza hayo alipokutana na wafanyakazi wa bandari.

Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment