Venus Williams amtupa nje Johanna Konta michuano ya Wimbledon


Venus akisherekea ushindiVenus akisherekea ushindi 

Matumaini ya Muingereza Johanna Konta kufika fainali za Wimbledon yamefutiliwa mbali baada ya kuchapwa na Venus Williams wa Marekani katika hatua ya nusu fainali.

Venus mwenye miaka 37 alicheza kwa umakini mkubwa zaidi na kushinda kwa seti 6-4 6-2.

Konta anayeshikilia nafasi ya sita kwa ubora duniani, alitegemea kufika fainali hizo na kuwa wa kwanza kufanya hivyo kwa Uingereza tokea mwaka 1977.
Konta anasema alitegemea upinzani mkali kutoka kwa VenusKonta anasema alitegemea upinzani mkali kutoka kwa Venus 

Matumaini pekee kwa Konta ni kuingia ndani ya tano bora kwa ubora.

Venus atachuana na Garbine Muguruza wa Hispania aliyemchapa Magdalena Rybarikova wa Slovakia kwa seti 6-1 6-1.
 
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment