Murray atupwa nje na Sam Querrey michuano ya Wimbledon

Muray hakua katika hali nzuri katika hatua za mwisho za mpambano dhidi ya QUerrey 

Bingwa mtetezi wa michuano ya Wimbledon Andy Murray amesukumwa nje ya mashindano hayo na Sam Querrey katika hatua ya nusu fainali.

Murray ambaye amekuwa na majeraha hakuweza kucheza vizuri katika mpambano huo.
Querrey, 29, ameshinda kwa seti 3-6 6-4 6-7 (4-7) 6-1 6-1 na kuwa Mmarekani wa kwanza kufanya hivyo tokea Andy Roddick alipofika katika hatua hiyo mwaka 2009.
QUerrey alikuwa katika kiwango bora kwenye mchezo huoQUerrey alikuwa katika kiwango bora kwenye mchezo huo 
Murray, 30, aliongoza awali lakini maumivu ya goti yalimfanya ashindwe kuuhimili mchezo.

Majeraha aliyoyapata pia Novak Djokovic yanamfanya Murray aendelee kushikilia namba moja.
Djokovic namba mbili kwa ubora duniani, alipaswa kushinda mchezo dhidi ya Tomas Berdych lakini majeraha ya kiwiko yakakatisha matumaini hayo.

 
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment