Majambazi wawapora fedha wafanyabiashara Nyampande, Sengerema

Watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi wakiwa na silaha za moto wamevamia katika kijiji cha Nyampande Wilayani Sengerema na kufanikiwa kupora pesa zaidi ya shilingi milioni tatu usiku wa kuamkia leo.

Wakizungumzia uvamizi huo wahanga wa tukio hilo ambao ni wafanyabashara wamesema kuwa wamesikia milio ya risasi ikisikika majira ya sasa saba usiku katika kijiji hicho na kupigwa butwaa, huku wakiwa kwenye majumba yao wakihofia kuuawa na majambazi hao.

Mwenyekiti wa kijiji cha Nyampande Salum Said Feleshi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kutaja majina ya watu walioibiwa mali zao na kubainisha kuwa jumla ya mali zilizoibiwa zinathamani ya zaidi ya sh.milioni 3.

Feleshi amesema kuwa uhalifu huo umewachanga kwani  katika maduka ya wafanyabiashara hao   kulikuwa na walinzi waliowajiri  wakiwa na silaha za moto na kusema kuwa tayari walinzi hao wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani Sengerema kwa mahojiano zaidi.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment