GARI LA ZIMAMOTO IRINGA LAZINDULIWA


Hatua hiyo ya uzinduzi wa gari la zimamoto msaada kutoka kwa Hanspope imekuja punde mara baada ya Gari la jeshi hilo la zimamoto kuanguka na kuharibika vibaya wakati likielekea kuzima moto Isimani wilaya ya Iringa vijijini  tarehe 23/04/2017  kwa  kukosa muelekea na kuanguka.

Akitoa taarifa wakati wa uzinduzi huo Kamanda wa Jeshi la zimamoto Kennedy Komba amesema, Mkoa wa Iringa una vituo vya zimamoto vinne huku kwa jiografia ya mkoa wa Iringa ulitakiwa kuwa na vituo 6 na kwasasa mkoa una gari moja tu la kuzima moto na la pili ambalo lilipata ajari.
 
Aidha kamanda amesema katika mkoa wa iringa mwaka 2015-2016 ulikua na matukio ya moto na maokozi takribani 110 ambapo matukio ya moto yalikua 90 na matukio ya maokozi yalikua 20 ambayo sawa na asilimia 1.1 na mwaka 2016-2017 matukio ya moto na maokozi yalikua 97 ambapo matukio ya moto yalikua 83 na maokozi yalikua 14 sawa na asilimia 0.97.

Amesema kuna changamoto nyingi zinazoikabili jeshi la zimamoto kuwa ni mpangilio wa mji hususani nje ya manispaa ya iringa na miundombinu kwa maana ya barabara . Kamanda amemshukuru Hanspope kwa msaada alioutoa.

 Kabla ya kukabidhi Gari hilo lenye uwezo wa kubeba maji lita 5000 ZAKARIA HANSPOPE amesema kwa sasa Manispaa ya Iringa inakua kwa kasi na hivyo kuna haja kuweza kukabiliana na hali hiyo na majengo makubwa yakiwa yanajengwa magari kama hayo yanahitajika zaidi kwa usalama wa mali za watu.
 
“Mimi nimezaliwa hapa Mkoani Iringa na kusoma hapa na baba yangu pia ameisha hapa hivyo wakati mwingine ni bora kurudisha fadhila kwa mkoa ambao umetokea kwa kuleta maendeleo. Alisema Hanspope.


Kamishna Jenerali wa zima moto Tanzania Kamanda Thobias Andengenye ameshukuru kwa kupatiwa msaada huo wa gari na amesema jeshi hilo lina upungufu wa vifaa vya kuzimia moto na huku vilivyopo pia ni vichakavu. 

Amesema katika kutatua changamoto hizo serikali kushirikiana na jeshi hilo la zimamoto wamekua wakitenga bajeti kwa ununuzi wa vifaa vya uokozi na kwa mwaka huu wametenga bajeti ya shilingi Bilioni 3 kwaajili ya kutatua changamoto hiyo.

 Kwa upande wake mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh Amina Masenza amemshukuru Hanspope kwa msaada huo na kumuomba kushirikiana nae katika kutatua matatizo mbalimbali ya kimaendeleo na kwamba mwanzo alishirikiana nae vizuri wakati timu ya lipuli ilipokosa msaada. 



Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment