Breaking: Mahakama yamuachia Mbunge Godbless Lema kwa dhamana

Mahakama Kuu Kanda ya Arusha leo imemuachia kwa dhamana Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema baada ya kukaa mahabusu kwa muda wa miezi mine.

Lema aliyekamatwa mapema mwezi Novemba mwaka jana amekuwa akikwama mara kwa mara kupatiwa dhamana katika kesi inayomkabili ya uchochezi dhidi ya Rais Dkt John Pombe Magufuli.

Mahakama imemuachi baada ya kutimiza masharti ya dhamana yaliyokuwa yakimtaka kuwa na wadhamini wawili na TZS milioni 1.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment