WATATU WAUAWA KWA MAPANGA MKOANI RUKWA



Watu  watatu  wa familia  moja  katika  kijiji  na  kata   ya  mfinga  Tarafa  ya  mto  wisa   wilaya  ya  Sumbawanga   mkoani   Rukwa wamefariki  dunia  baada   kukatwa   katwa  na mapanga   katika  sehemu  mbalimbali  za mili  yao  kutokana na  imani  za kishirikina.

Tukio  hilo  la  kushangaza  limetokea  baada  ya watu  wasio  julikana  kuwavamia  watu  hao  nyumbani  kwao   na  kisha kuvunja mlango  wa  nyumba  yao  na  kuwakatakata  na mapanga   na  kutokomea  kusiko  fahamika   kutokana na  imani  za  kishirikina.

Kamanda  wa  polis mkoani  Rukwa   geoge  samba  kyando amesema    chanzo  cha  tukio  ni  imani  za  kishirikina  ambapo  watu   hao  walivunja  mlango  kisha    kufanya  unyama  huo  na  kuwataja   marehemu  kuwa  ni JOACHIM KAYANDA ,umri miaka 60,EVERINA MWANAKATWE ,umri miaka 47 na EMMANUEL KAYANDA, umri miaka 27 wote wakiwa ni wakazi wa kijiji cha Kipa na  kusema  Watuhumiwa watano wanashikiliwa  kwa  mahojiano  zaidi na watafikshwa mahakamani pale uchunguzi utakapokamilika.

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa Kamishna Msaidizi wa Polisi GEORGE SIMBA KYANDO   amewataka wananchi kuacha  tabia  ya   kujichukulia  sheria  mkononi.

Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment