AUBAMEYANG AACHWA NJE KATIKA KIKOSI CHA DORTMUND

Mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang ametemwa katika kikosi cha timu hiyo kutokana na maswala ya ukosefu wa nidhamu.
Mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang ametemwa katika kikosi cha timu hiyo kutokana na maswala ya ukosefu wa nidhamu.

Ripoti kutoka Ujerumani zinasema kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 alichelewa katika mazoezi lakini Aubemayang anasema kuwa alikasirishwa na uamuzi huo.

Aubameyang hatashirikishwa katika mechi dhidi ya VFB Stuttgart siku ya Ijumaa.

Dortmund ilitangaza kumsimamisha kwa muda mchezaji huyo ikijibu maswali ya mashabiki wake katika Twitter, lakini haikuelezea sababu ya hatua hiyo.

Raia huyo wa Gabon pia alisimamishwa kwa muda mwaka uliopita baada ya kuelekea Italy bila rukhusa ya klabu hiyo.

''Sielewi ni kwa nini, nilizuiwa kuelekea Milan kwa sababu sikuheshimu sheria , lakini wakati huu nimekasirishwa sana , sikutaka kuwasili nikiwa nimechelewa'', aliambia gazeti la Bild nchini Ujerumani.

Dortmund imepoteza pointi tatu katika mechi zake nne na hivyobasi kushuka katika jedwali la ligi pointi sita
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment