Wenger: Alexi Sanchez hajasema anataka kuondoka

Arsene Wenger kulia 
Mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez hajamwambia mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger kwamba anataka kuondoka katika klabu hiyo , kulingana na mkufunzi huyo ambaye anatarajia mchezaji huyo wa Chile kukamilisha kandarasi yake.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 amesalia na mwaka mmoja katika kandarasi yake na Arsenal.

Hatahivyo imeripotiwa kwamba Sanchez angependa kujiunga na wapinzani wa Arsenal Manchester City .
Alipoulizwa iwapo Sanchez alimwambia kwamba angependelea kuondoka , rais huyo wa Ufaransa amesema kuwa hapana.

Wenger aliongezea: Wachezaji wana kandarasi na tunawatarajia kuheshimu kandarasi zao , hilo ndio tunalotaka.

Sanchez alijiunga na Arsenal kutoka Barcelona kwa kitita cha pauni milioni 35, 2014.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment