MAYWETAHER AMWAGIA DOLA MCGREGOR, ILA MAJIBU ALIYOPEWA HANA HAMU!

Floyd Mayweather and Conor McGregor square up at the Brooklyn Center, New York City, ahead of their bout on August 26 
BONDIA Floyd Mayweather usiku wa jana alimwagia noti za dola za Kimarekani mpinzani wake, Conor McGregor katika mwendelezo wa promosheni ya pambano lao Agosti 26, mwaka huu.
 
Katika mkutano huo wa tatu kuwakutanisha uso kwa uso kwa ajili ya ziara ya promo la pambano lao, Mayweather alimuita McGregor muachaji akimanisha hawezi kuvumilia kumalizia jambo na kisha akamrushia noti za dola akisema; "Naendesha shoo, hi ni** yangu na na ninamwagia dola moja huyu****."
 
Baada ya siku tatu za promosheni, baadhi wamesema wawili hao wanakwenda nje ya mstari, wakati pia wawili hao wameshindwa kuheshimiana.
 
Bondia Floyd Mayweather akijivuta pembeni baada ya kumwagia dola mpinzani wake, Conor McGregor usiku wa jana

Wakati wawili hao waliibuka watulivu safari hii, hakukuwa na msisimko hadi Mayweather aliposogea jukwaani na 'kulianzisha'. 
 
McGregor alimkandia Mayweather "uso kwa uso" mwanzoni kwa kumuambia anaelekea kufilisika kama rafiki yake '50 Cent'. "Amefilisika na wewe unaelekea.'
 
Nyota huyo wa Ireland kisha akampa Mayweather albamu mpya ya Jay Z na kumuambia ampe 50 na amuambie 'blanco amekutumia'. 
 
"Hawajui mimi ni nusu mweusi? Mimi ni nusu mweusi haswa," alisema ili kujikosha na tuhuma za ubaguzi wa rangi alizokwishaanza kutupiwa na kwenda kucheza na shabiki wake wa kike mweusi.
Dana White (second right) steps in as things get heated between the two fighters as the slurs started almost immediately
 
Baadaye Mayweather akakamata kipaza sauti tena na kusema: "Unajua nini, ninakuka? ninanuka****'.
 
Kisha akaugeukia umati kuuambia umnyooshee kidole 'muachaji' kabla mistari ya wimbo 'Baby Tap Out' haijaanza kusikika kwenye spika kubwa. 
 
Mbabe huyo mwenye umri wa miaka 40 kisha akaanza kumtupia noti za dola McGregor ambaye alijibu kwa mshituko: "Zote ni dola moja moja! Ziko wapi fedha halisi?'
Mayweather laps up the noise from the thousands of fans as McGregor, dressed extravagantly, looks on
 
"Kwa sababu huo ndiyo utajiri wako wote," Mayweather akakasirika.
 
Mmarekani huyo kisha akaonekana kutaka kumvaa mpinzani wake, kabla ya timu yake kumuondoa McGregor. Timu ya bondia wa Ireland inayowahusisha Dillon Danis na Owen Roddy, nayo haraka ikaingia, huku umati wa 19,000 uliokuwepo ukumbini ukishangilia.
 
Upinzani wao utaendelea Uwanja wa Wembley mjini London, Ijumaa jioni.
 
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment