Wafungwa 12 wapigwa risasi Papua New Guinea

Mwaka 2016 inadaiwa kuwa wafungwa walivamia lango kuu la gereza hilo
Maafisa wa magereza nchini Papua New Guinea, wamewapiga risasi na kuwauwa wafungwa 17, ambao walivunja gereza na kutoroka siku ya Ijumaa.
Polisi wamewatia mbaroni wafungwa watatu, huku wakiendelea kuwasaka wengine 50 ambao bado hawajulikani waliko tangu kutokea kwa kisa hicho katika gereza la Buimo katika mji wa Lae.
Polisi wanasema kuwa, wengi wa wafungwa waliotoroka walikuwa wahalifu sugu.
Idara ya usalama nchini humo imewatahadharisha raia kuwa macho na watoe taarifa kwa vyombo vya usalama pindi wakiwaona wafungwa hao.
Gereza hilo la Buimo huwa na msongamano mkubwa wa wafungwa na uchafu na mwaka jana wafungwa 12 waliuawa baada ya kujaribu kutoroka.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment