Wachezaji wa kikosi cha Zambia wakishangilia baada ya ushindi dhidi ya Iran
Michuano ya kombe la dunia la vijana
chini ya umri wa miaka 20 inaendelea kushika kasi huko nchini Korea ya
kusini ikiwa katika ngazi ya makundi.
Kwenye kundi D Afrika ya kusini walichapwa na Italia kwa mabao 2-0, huku Uruguay wakiwafunga Japani kwa 2-0.
Kikosi cha timu ya taifa ya Uruguay
Michuano hiyo inaendelea tena leo katika kundi E Ufaransa watacheza na Vietnam, na New Zealand wakipepetana na Honduras.
Katika kundi F Ecuador wataonyesha ubavu na Saudi Arabia, huku Senegal wakicheza na Marekani.
0 Maoni:
Post a Comment