Guterres: Mazingira yameimarika Somalia

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antinio Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, ameambia kikao cha kimataifa kinachojadiliana hatma ya Somalia kuwa mazingira nchini Somalia hivi sasa yameimarika na kwamba taifa hilo linaweza kufaulu katika yale linalotaka kufanya.
Amesema nchi hiyo kwa sasa ina serikali ambayo inaweza kuaminika na mipango yenye maana.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema Jumuia ya Kimataifa ina nafasi kubwa kuisaidia Somalia.
Hata hivyo Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohamed Farmajo ameonya kuwa mapambano dhidi ya wapiganaji wa Al Shabaab yanaweza kuendelea kwa miongo kadhaa iwapo vikwazo vya silaha havitaondolewa.
Mkutano huo wa siku moja ulizungumzia pia tatizo linaloikabili Somalia la athari za ukame ambazo zinageuka kuwa baa la njaa.
Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment