Man united hali bado tete

goli 
Mashetani wekundu wa Manchester wamendelea na mwendo wa kukuasua katika ligi kuu ya England baada ya kuambulia sare ya goli 1-1 na Everton katika dimba la Old Traford.

Beki wa Everton Phil Jagielka ndie aliyeanza kuzifumania nyavu za Man United katika dakika ya 22, ya mchezo kabla ya Zlatan ibrahimovic kusawazisha goli hilo kwa mkwaju wa penati katika dakika za lala salama.

Leicester City wakicheza katika dimba lao la king power walichomoza na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Sunderland kwa mabao ya Islam Slimani na Jamie Vardy.
vard 
Wanajeshi wa wa njano wa Watford wakaibuka na ushindi wa mabao 2 - 0 dhidi ya West Bromwich, mabao ya Watford yakifungwa na Troy Deeney na Mbaye Niang.

Nao Burnley wakataka nyumbani kwa ushindi wa goli 1 - 0 dhidi ya Stoke City Jj

Share on Google Plus
Ahsante kwa kutembelea site yangu, unaweza kunicheki kwenye mitandao ya kijamii kwa kubonyeza icons juu kulia na kunipata moja kwa moja kwenye Facebook, Twitter na Instagram...Endelea kuwa karibu yangu ili uweze kufikiwa na chochote kinachonifika.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment